NAKUPENDA EWE WANGU 1. Wewe ndie nyota yangu,usiku wamulikia. Uniachi peke yangu,ukanacha ninalia. Nikabaki peke yangu,mbali ukanikimbia. Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda. 2. Wewe ndie mwezi wangu,usiku waangazia. Ewe ndie taa yangu,mwanga wanimulikia. Wewe ndie nuru yangu,wewe ndo langu pazia. Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda. 3. Wewe ni asali wangu,nyuki sitowafukuza. Kuvunja mzinga wangu,ni jambo nisiloweza. Nikabaki peke yangu,ulimwengu kuniweza. Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda. 4. Ewe ndio shuka langu,lanilinda kwa baridi. Wewe ndie koti langu,daima sitokaidi. Takulinda vazi langu,ili nije kufaidi. Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda.
NIELEZE nambie swahiba;nipate elewa kuchomwa na mwiba;si hadi kulewa kwa nini umevimba;mi sijaelewa..... nieleze!!! nambie habiba;nijue kwa nini kutwa umevimba;hatuelewani na hali mkosa;ni wewe si mimi nambie!!! kuwa na hiyana;si vema ujue alo muungwana;hafichi mwenziie alapo banana;humwita mwezie nambie!!