Skip to main content

NAKUPENDA EWE WANGU

 NAKUPENDA EWE WANGU

1. Wewe ndie nyota yangu,usiku wamulikia.
Uniachi peke yangu,ukanacha ninalia. 
Nikabaki peke yangu,mbali ukanikimbia. 
Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda.

2. Wewe ndie mwezi wangu,usiku waangazia. 
Ewe ndie taa yangu,mwanga wanimulikia. 
Wewe ndie nuru yangu,wewe ndo langu pazia. 
Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda. 

3. Wewe ni asali wangu,nyuki sitowafukuza.
Kuvunja mzinga wangu,ni jambo nisiloweza.
Nikabaki peke yangu,ulimwengu kuniweza.
Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda.

4. Ewe ndio shuka langu,lanilinda kwa baridi. 
Wewe ndie koti langu,daima sitokaidi. 
Takulinda vazi langu,ili nije kufaidi.
Nakupenda ewe wangu,kwengine siwezi kwenda.

Comments

  1. limekaa poa haswa ukizingatia katika kudumisha upendo na mapenzi ya watu waliopendana

    ReplyDelete
  2. Imeweza,,ila buni hisia kuiongeza uzito

    ReplyDelete
  3. Umeweza mtunzi hapo lakini ongeze kwenye mnato wa hisia

    ReplyDelete
  4. Mashaallaah lipo bomba sana nmelipenda

    ReplyDelete
  5. However, you should be aware that when you play gambling, you risk losing your money. Be prudent in your assessment of all potential dangers. Consider world777 gambling to be nothing more than a game. Don't get too worked up if you lose, because in an online gambling game, winning and losing can happen at any time.

    ReplyDelete
  6. First I appreciate your work very much. I read your post carefully and I must say that you are doing a great job by sharing your thoughts with us. Please check out does starbucks take ebt

    ReplyDelete
  7. A significant site you have got here... It's difficult to find excellent writing like yours these days. survival fund

    ReplyDelete
  8. Find Best Way How to Index backlink fast. For this Technique You will get Instant approval Result

    ReplyDelete
  9. https://imageshack.com/user/mondalldesign

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

PENZI

PENZI Penzi njia ya adhabu, sina budi kuipita, Tena ina nyingi tabu, ila siwezi iwata, Leo naomba jawabu, ni lini nitakupata? Penzi pia ni safari, ya hatari na salama, Kuna wakati shuari, mara upepo wavuma, Sote tuwe wasafiri, katu tusirudi nyuma. Penzi ni kama misimu, iliyo ndani ya mwaka, Kwa fuuza haidumu, kipupwe mara masika, Kuna muda ufahamu, majani hupukutika. Penzi ni kama bahari, hutulia huchafuka, Hupita mumo vihori, meli kubwa kadhalika, Hivyo lataka hadhari, sivyo tupu kusumbuka. Penzi mithili ya jua, huchomoza na kuzama, Haya tusipoyajua, hakika twaenda kwama, Hapa tamati natua, katika wako mtima.

MPENZI RUDI NYUMBANI

MPENZI RUDI NYUMBANI 1. Mie nipo fikirani, mawazo yangu ya mbali, Sijui mkosi gani, nikaibinua stuli, Matone ya zafarani, katika kanzu na shali, Si urongo ni kweli, mwenzako sina amani. 2. Mekukumbuka fulani, usiku mie silali, Sijiwezi tabaani, siioni afadhali, Tonge halendi kinywani, zanipwaya suruali, Nimekonda kwelikweli, thama ni wewe jamani. 3. Siko vizuri kitwani, nenda rukwa na akili, Mwenzako kiza sioni, sipokuwa Ziraili, Roho yangu ishakani, kupona sina dalili, Sihitaji sipitali, namtaka wangu hani. 4. Mambo hayendi kazini, zimesimama shughuli, Hunitoki akilini, kutwa naona thakili, Naenda ovyo njiani, nikiwa na idhilali, Peke una ikibali, kupunga wangu shetani. 5. Nyonda hebu pulikani, sinitende ukatili, Hutotoka hatiani, roho ikiwacha mwili, Nakwambia si utani, hulikwepi zigo hili, Niikikata kauli, wapata faida gani? 6. Sita nafunga uneni, fahamu huna badili, Turudi kama zamani, makosa nayakubali, Nyongo mkalia ini, fahamu sinayo hali. Hebu fanya kulla hali, mpenzi rudi nyum...